Gonzalo Higuain alifunga mabao mawili, huku bao lingine likifungwa na Paulo Dybala, na kuifanya Juve kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi na mahasimu zao, AS Roma.
Juventus, maarufu kama Kibibi kizee cha Turin imedhamiria kuweka rekodi ya kushinda ubingwa wa Scudetto, kwa mara sita mfululizo, huku ikiwa ina mchezo mmoja mkononi.