Ijumaa , 10th Sep , 2021

Los Angeles Lakers wamefanikiwa kumsajili mchezaji wa kati, DeAndre Jordan kutoka Brooklyn Nets, na taarifa hii imetangazwa leo na Meneja Mkuu wa timu hiyo Rob Pelinka, kwa makubaliano ya pande mbili ambayo hayajawekwa hadharani.

DeAndre Jordan akiwa kwenye majukumu yake na waajiri wake wa zamani Brooklyn Nets.

Mkongwe wa miaka 13 katika ligi NBA, Jordan alicheza michezo 57 msimu ulipopita, akianza mara 43 akiwa na wastani wa alama 7.5, ribaundi 7.5, usaidizi wa 1.6 na vizuizi 1.1 kwa dakika 21.9, huku akipiga pointi bora ya asilimia 76.3 (190 -249).

Jordan ndiye kiongozi wa wakati wote wa NBA katika asilimia ya vitupwe vya pointi uwanjani , akiwa amepiga asilimia 67.4 (3527-5234) kutoka uwanjani wakati wote na ndiye mchezaji pekee katika historia ya NBA na misimu mingi akipiga pointi nyingi zaidi ya asilimia 70 uwanjani.

Jordan ameshiriki mara moja na kuchaguliwa mara tatu katika michezo ya NBA All-star, pamoja na uteuzi mmoja wa timu ya kwanza ya msimu mwaka 2016 na chaguzi mbili za timu ya tatu mwaka 2015 & 2017.

Pia iliongoza ligi hiyo katika ribaundi misimu mfululizo kutoka 2013-15. Pia alitajwa katika Timu ya Kwanza ya Walinzi mnamo 2015 na 2016 na akaisaidia Marekani kushinda medali ya dhahabu kwenye Olimpiki za 2016 huko Rio de Janeiro.