Haji Manara na Patrick Aussems
Mchezo huo uliopigwa katika Uwanja wa Taifa, ilishuhudiwa Yanga ikiwazuia Simba kwa ushindi mwembamba wa bao moja kwa sifuri.
Kufuatia matokeo hayo, Afisa Habari wa Simba, Haji Manara ambaye hakuwepo nchini jana wakati wa mchezo, amewaomba mashabiki wa klabu hiyo kutulia na kuungana kwa ajili ya mechi zilizobakia.
Kwa upande wake, aliyewahi kuwa kocha wa klabu hiyo, Patrick Aussems amesema kuwa amesikitishwa na matokeo hayo, lakini akisema kuwa alitarajia kwa hicho kilichotokea.
Sorry ( but not surprised ) to hear about the defeat against Yanga ... it's a very sad day for the players and all Simba fans !!! pic.twitter.com/iBOAesADsh
— Patrick Aussems (@PatrickAussems) March 8, 2020