Martin Odegaard akiwa na timu ya Real Sociadad katika mechi ya la liga dhidi ya Real Madrid
Wameamua kumrudisha mchezaji wao raia wa Norway Martin Odegaard aliyekuwa anacheza Real Sociedad kwa mkopo, Martin mwenye umri wa miaka 21 pamoja na kusajiliwa akiwa kinda amekuwa akitolewa kwa mkopo wa muda mrefu
Odegaard alisajiliwa na Real Madrid akiwa kinda wa umri wa miaka 16 kutoka nyumbani kwao Norway na wengi waliamini kipaji chake ni cha juu hadi kufananishwa na akina Messi na Cristiano Ronaldo lakini haikuwa hiyo
Msimu huu akiwa na Real Sociedad amefanya vyema kwa kutoa mchango mkubwa wa moja kwa moja hadi kupelekea Zidane kumrejesha tena katika kikosi.