Aly Soumah ambaye alirudishwa kwao baada ya kugundulika kuwa alidanganya kwenye taarifa zake na kutokidhi vigezo vya kuwa kwenye kikosi hiko, alipata ajali ya gari katika eneo la Kindia nchini kwao Guine na baadae kufariki.
Mchezaji kudanganya umri
Kutokana na kipimo cha MRI kuonesha kuwa Aly kavuka umri, alilazimika kurudishwa kwao kabla ya mchezo wa ufunguzi wa AFCON kati ya timu yake ya Taifa ya Guinea katika uwanja wa Chamazi Dar es Salaam dhidi ya Cameroon ambapo katika mchezo huo Cameroon walishinda 2-0.