Bernard Morrison akisaini mkataba Simba
Kupitia kurasa rasmi za Simba Sports Club kwenye mitandao ya kijamii mchana wa leo Agosti 8, 2020 wameweka picha za Morrison akisaini pamoja na ujumbe mfupi 'Morrison is Red'.
MORRISON IS RED #NguvuMoja pic.twitter.com/c1YwlNczOP
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) August 8, 2020
Morrison ambaye ni raia wa Ghana anakumbukwa kwa kuifunga Simba goli pekee lililoipa ushindi Yanga kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara Machi 8, ambapo Yanga ilishinda 1-0.