Goli la Mbwana Samatta
Hiyo imekuja baada ya kuonesha kiwango kikubwa katika mchezo wa marudiano wa Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Liverpool uliopigwa katika dimba la Anfield, ambapo Samtta alifunga bao safi la kichwa.
Kwa mujibu wa vipengele vya mkataba wake, klabu yoyote inayomtaka mshambuliaji huyo inatakiwa kutoa kiasi cha Pauni 10 milioni ili kumng'oa kwa mabingwa hao wa Ubelgiji.
Samatta (26) alikuwa mfungaji bora namba mbili wa ligi kuu ya soka ya Ubelgiji msimu uliopita, akifunga mabao 25 na msimu huu tayari amefunga mabao sita katika mechi 13 za mashindano yote alizocheza.