Jumatatu , 4th Oct , 2021

Promota wa bondia Tyson Fury, Frank Warren amesema endapo Fury atapata ushindi wa Mkanda wa Ubingwa uzito wa juu wa WBC dhidi ya Deontay Wilder  Oktoba 10, 2021 jijini Las Vegas nchini Marekani basi pambano linalofuata la Fury litachezwa Engalnd.

Tyson Fury baada ya kushinda mkanda wa ubingwa wa uzito wa juu WBC kwa kumpiga Deontay Wilder Februari 2020 nchini Marekani.

Kauli ya Warren imekuja baada ya Fury kusaini mkataba mnono na ESPN uliomlazimu mapambano yake manne yafanyike nchini Marekani likiwemo lile la mchezo wa kwanza uliomalizika kwa sare na Deontay Wilder mwaka uliopita.

Fury ambaye mara yake ya mwisho pambano lake kufanyika nchini England ilikuwa ni mwaka 2018,  anatazamiwa kupambana kati ya Oleksander Usyk  au Anthony Joshua licha ya pambano la Joshua kuonekana kuwa hai zaidi.