Jumamosi , 23rd Jun , 2018

Klabu ya Real Madrid imeingia mkataba wa miaka 6 na kinda Andriry Lunin kutoka Zorya Luhansk ya Ukraine, kinda huyo mwenye umri wa miaka 19, amejiunga na Madrid kwa lengo la kumpiga tafu kipa wa sasa Keylor Navas.

Golikipa Andriry Lunin akiwa uwanjani

Madrid imeendelea na usajili huo baada ya kumalizana na kinda mwingine Rodrygo Goes kutoka Santos FC ya Brazil, Kocha Mkuu mpya wa kikosi cha Madrid ameamua kuanza kukisuka upya kikosi chake baada ya Zinedine Zidane kuondoka.

Ujio wa Luhansk unaweza ukawa umefuta rasmi ndoto za Madrid kuendelea kumuhitaji kipa wa Manchester United, David de Gea ambaye walikuwa wanampigania kwa udi na uvumba.

Kipa David de Gea ndiye anayeonekana sana kuwindwa na Kocha huyo kwa sasa, ambapo kabla ya kuitumikia Manchester United ameitumikia pia Atletico Madrid ambayo aliidakia michezo zaidi ya arobaini na tano.