Jumapili , 10th Nov , 2019

Kuelekea mchezo wa Ligi Kuu soka nchini England kati ya Vinara wa ligi Liverpool dhidi ya Manchester City, wanaoshika nafasi ya tatu utakaopigwa usiku wa leo Novemba 10, 2019, haya ni mambo kadhaa ya kuyajua.

Sergio Kun Aguero na Pep Guardiola

Licha ya umahiri wake wa kupasia nyavu, Sergio Aguero ambaye pia ni mfungaji wa muda wote wa Man City, hajafanikiwa kupata goli katika mechi 7 alizocheza kwenye uwanja wa Anifield.

Tofauti na mechi 7 alizocheza dhidi ya Liverpool kwenye uwanja wa Etihad ambapo amefunga magoli 7, kwa maana ya goli 1 kila mchezo.

Kwa upande mwingine Liverpool ina rekodi nzuri zaidi inapocheza na Bingwa mtetezi wa Ligi kuu ya England ambapo ndiyo timu iliyoshinda mara nyingi zaidi inapokuna na bingwa. Imeshinda mechi 21.

Kwasasa kiungo wa Liverpool Fabinho, ndio anaongoza kwa kumiliki zaidi mpira akiwa na wastani wa Jumla ya 245, kwenye Ligi kuu pamoja na Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Manchester City inamkosa mlinda mlango wake namba moja Ederson Moraes ambaye ni majeruhi, hivyo Claudio Bravo atakuwa na dhamana ya kusimama langoni.

Liverpool ina pointi 31 kileleni baada ya mechi 11, ikiwa katika nafasi ya kwanza wakati Man City ambao ni mabingwa watetezi wana pointi 25 katika mechi 11 wakiwa nafasi ya 4.

Mchezo huo unatarajiwa kuanza saa 1:30 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.