Jumatatu , 17th Feb , 2020

Ligi Kuu Tanzania bara ipo katika mzunguko wa 22 kwa timu takribani 18, kwa Yanga ikiwa katika mzunguko wa 20 huku Namungo FC ikiwa katika mzunguko wa 21.

Kikosi cha Ndanda FC

Klabu ya Ndanda imeweka rekodi ya kipekee kwa klabu za ligi kuu msimu huu, ambapo mpaka sasa haijafungwa katika michezo mitano mfululizo lakini rekodi nzuri zaidi ni kutoruhusu bao lolote la kufungwa katika mechi hizo.

Ndanda imeshinda mechi nne, dhidi ya Singida United (1-0), Mwadui FC (2-0), Mbao FC (3-0) na Alliance FC (1-0), huku ikipata sare moja ya bila kufungana dhidi ya Namungo FC na kuifanya kuwa klabu ya kwanza kuweka rekodi hiyo katika msimu wa 2019/20.

Licha ya rekodi hiyo nzuri ya Ndanda hivi karibuni, bado ipo katika hatari ya kushuka daraja, kwani mpaka sasa ipo katika nafasi ya 15 ikiwa na pointi 22. Timu nne zitashuka daraja msimu huu moja kwa moja na timu mbili zikitakiwa kucheza hatua ya mtoano kwa ajili ya kusalia kwenye ligi.