John Bocco akisaini mkataba
John Bocco amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Simba kuanzia msimu ujao, ikiwa ni baada ya kuonesha ubora mkubwa katika msimu uliomalizika.
Taarifa hiyo imetolewa kupitia kurasa rasmi za klabu hiyo, ikiwemo Twitter.
John Bocco amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuichezea klabu yetu. Bocco ambaye alikuwa mchezaji bora wa Simba na Ligi Kuu kwa msimu wa 2017/18 na Mshambuliaji Bora kwa msimu wa 2018/19 amefunga jumla ya mabao 30 ya Ligi katika misimu miwili. #NguvuMoja pic.twitter.com/6f867oWEU2
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) June 10, 2019
Katika msimu wa 2018/19, John Bocco ameifungia Simba mabao 16 ya ligi.