Kocha wa Simba Patrick Aussems
Inadaiwa kuwa mwisho wa msimu huu wa 2018/19 Chilunda ambaye alikuwa anacheza Tenerife ya ligi daraja la kwanza Hispania, amevunja mkataba na timu hiyo.
Chilunda alikuwa akicheza kwa mkopo wa miaka miwili akitokea Azam FC, lakini anaelezwa kuvunja mtakaba wake baada ya msimu wa kwanza mambo kutomwendea vizuri ikiwemo kukosa nafasi ya uhakika ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza.
Baada ya taarifa hizo za Chilunda kuvunja mkataba, Simba imeelezwa kuwa na nia ya kumsajili mshambuliaji huyo ambaye amewahi kuwa mfungaji bora wa klabu bingwa Afrika mashariki na kati.
Chilunda kwa sasa yupo kwenye kambi ya Taifa Stars inayojiandaa kwa ajili ya maandalizi ya fainali za AFCON 2019, zitakazofanyika nchini Misri kuanzia Juni 21 hadi Julai 19.