Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau
Hayo yamethibitishwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Wilfred Kidau katika mkutano na wanahabari leo, makao makuu ya shirikisho hilo, Ilala Jijini Dar es Salaam.
Kidau amesema kuwa hatua hiyo imekuja kutokana na taarifa ya mabadiliko ya katiba waliyopokea kutoka FIFA ya kuwataka kuunda upya Kamati za Utendaji na nafasi zingine ndani ya shirikisho hilo.
"FIFA walikuja hapa wakataka kukutana na wadau ambao mabadiliko hayo ya katiba yanawahusu. Kwenye maeneo ambayo ni ya lazima tufanye, wametaka tupunguze ukubwa wa Kamati yetu ya Utendaji", amesema Kidau.
"Wametaka tuwe na vikao vya Kamati ya Utendaji kila baada ya miezi miwili badala ya miezi mitatu. Pia wajumbe wa Kamati yetu ya Utendaji ni wengi karibia 130 wakati wenzetu Nigeria wanapigiwa kura na wajumbe 39", ameongeza.
Pia katika mabadiliko hayo ya uongozi, Wilfred Kidau amesema kuwa TFF imemteua aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura kuwa Mkurugenzi mpya wa Habari na Masoko wa shirikisho hilo.
#MICHEZO Kamati ya Utendaji ya TFF imemteua Boniface Wambura kuwa Mkurugenzi mpya wa Habari za Masoko wa shirikisho hilo la soka.
Wambura alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Ligi kabla ya kumaliza muda wake hivi karibuni. pic.twitter.com/OvqRpEsj0B
— East Africa TV (@eastafricatv) October 16, 2019
Pamoja na hayo, TFF pia imemteua kocha Oscar Mirambo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa shirikisho hilo.
#MICHEZO Shirikisho la soka Tanzania TFF limemteua Oscar Mirambo kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa shirikisho hilo.
Oscar Mirambo alikuwa kocha wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, kabla ya kujiuzulu. pic.twitter.com/YDcpnjBZdQ
— East Africa TV (@eastafricatv) October 16, 2019