Jumamosi , 23rd Mar , 2019

Timu ya taifa ya Uganda wameweka wazi kuwa wamepanga kumaliza vizuri hatua ya makundi, kuwania kufuzu fainali za AFCON 2019, ambapo watacheza na Tanzania Jumapili hii.

Emmanuel Okwi na baadhi ya wachezaji wa Uganda

Uganda ambao tayari wameshafuzu fainali hizo zitakazofanyika nchini Misri, wamesisitiza kuwa wanataka kumaliza vizuri wakiwa juu ya kundi L.

Kupitia ukurasa wa Instagram wa timu ya taifa ya Uganda, (Uganda the Cranes), wameeleza nia yao ya kushinda mchezo wa mwisho. ''Tuonyeshe uwezo wa juu zaidi katika kumaliza hii hatua'', wameandika.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

Let us finish this on a high note. #AFCON2019Q #TANUGA.

A post shared by Uganda Cranes (@ugandacranes) on

Uganda wameshinda mechi 4 na sare moja katika mechi zao 5 za Kundi L, hivyo kufikisha pointi 14 kileleni huku wakifuatiwa na Lesotho na Tanzania zenye pointi 5 wakati Cape Verde wana pointi 4.

Tanzania inahitaji ushindi ili kufuzu AFCON inayoanza mwezi Juni, lakini itasubiri matokeo ya Cape Verde na Lesotho ambapo inabidi Lesotho ifungwe au kutoa sare.