Victor Wanyama
Wanyama alisajiliwa na Spurs kutokea Southampton mwaka 2016 na kufanikiwa kuichezea michezo 69, akifunga mabao sita na mafanikio makubwa aliyoyapata ni kumaliza nafasi ya pili katika Ligi Kuu nchini Uingereza pamoja na kikosi chake kufika fainali ya Klabu Bingwa Ulaya msimu uliopita.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Wanyama ameandika ujumbe wa kuishukuru Spurs kwa kipindi chote cha miaka minne alichohudumu na kikosi hicho.
I want to thank @SpursOfficial fans for all the support over these past years,we have shared great times together from finishing 2nd in EPL to reaching the champions league finals,I will always be grateful for having be able to play for @SpursOfficial #COYS pic.twitter.com/Wtv3lxM1v5
— Victor Wanyama (@VictorWanyama) March 4, 2020
Amejiunga na klabu ya Montreal Impact inayoshiriki Ligi kuu ya nchini Marekani (MLS), chini ya mchezaji nguli wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa, Thierry Henry.