Jumatano , 31st Jul , 2019

Klabu ya soka ya Yanga imewapiku mahasimu wao wa jadi Simba katika kutambulisha wimbo rasmi wa klabu kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu na michuano ya Kimataifa.

Mashabuki wa Simba na Yanga

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Yanga imetambulisha wimbo wake rasmi utakaotumiwa katika michuano mbalimbali kuanzia msimu huu, na kusisitiza kuwa ni wajibu wa wanachama na mashabiki kuufahamu wimbo huo.

Wimbo huo wa Yanga utaanza kutumika katika mchezo wao wa Kimataifa wa 'Wiki ya Wananchi', Agosti 4 dhidi ya Kariobangi Sharks ya Kenya.

Mahasimu wao Simba waliahidi kutoa wimbo wao rasmi wa klabu ifikapo Agosti 3, 2019, wimbo ambao utaanza kutumika katika mchezo wao wa Kimataifa wa Simba Day, Agosti 6 dhidi ya Power Dynamo ya Zambia.