
Waziri wa TAMISEMI George Simbachawene
Simbachawene ameyasema hayo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha EAST AFRICA BREAK FAST kuifafanua kuhusu tishio la chama cha walimu nchini kuitisha mgomo nchi nzima kushinikiza serikali kuwalipa madeni yao.
“Mimi sijasikia tangazo lao la mgomo ila kusema kweli hakuna siku madeni ya walimu yataisha kabisa, tunachokifanya kwa sasa ni kumalizia uhakiki na kwenye uhakiki unakuta walimu wanaonesha wanaidai serikali ila ukiangalia na kukagua wengine wanakimbia, ila tukimaliza tutalipa kulingana na bajeti” Amesema Simbachawene.
Aidha Waziri amesisitiza kuwa changamoto ya walimu kukimbia zoezi la uhakiki husababisha muda kutumika zaidi kwa kuwa serikali haiwezi kutoa fedha zake bila kufanya uhakiki wa kina.
Pamoja na hayo Rais wa Chama cha Walimu nchini (CWT) Gratian Mukoba amesema serikali isipojitokeza hadharani na kutaja ni lini watayalipa, wataitisha mgomo nchi nzima.