Tuesday , 26th May , 2020

Najua kila mtu ana kigezo chake na uchaguzi wake pale anapompenda au kumtamani mtu yeyote ili kuwa naye kwenye mahusiano, mapenzi au kwenye ndoa kabisa.

Msanii wa filamu Jacqueline Wolper

Sasa EATV & EA Radio Digital, imepiga stori na msanii wa filamu na mfanyabiashara Jacqueline  Wolper, ambaye amesema hawezi kuwa na uhusiano na mwanaume mzuri au bishoo ila anapendelea watoto wa Kiswahili.

"Serious kabisa huwa sipendagi wanaume mabishoo, napenda wanaume ma-gangster au watoto wa kiswahili ndiyo mikato yangu, kwa sababu anajua nini maana ya maisha na sio bishoo kwenye kufanya chochote chenye kumuingizia riziki na  hiyo ndiyo maana yangu, huwezi kunikuta nipo kwenye mahusiano na mtoto mzuri kwanza siwazimii naona wananipotezea muda" amesema Wolper.