Marcus Rashford akishangilia moja ya bao aliloifungia klabu yake.
Rashford anatarajiwa kutunikiwa tuzo hiyo kutokana na mchango wake kwa jamii na mafanikio kwenye soka hivyo kuingia katika rekodi kutokana na umri wake mdogo.
Tuzo hiyo inatokana na kampeni yake dhidi ya umasikini , ikiwemo mapendekezo yake kwa serikali na taasisi mbalimbali kuwasaidia vijana mashuleni wanaotoka katika familia duni kwa mahitaji mbalimbali ikiwemo chakula.
Marcus Rashford ni zao la timu ya Manchester United ambayo alijiunga nayo akiwa mdogo na hatimaye kupandishwa timu ya wakubwa , na kwa sasa anatoa mchango mkubwa sana katika timu hiyo.