Msanii Mzee Yusuph kushoto, kulia Rich Mavoko
Kwa upande wa Rich Mavoko alikuwa kimya miezi saba bila ya kuachia kazi mpya, kuonekana kwenye shughuli za burudani, mahojiano na kutotumia mtandao wa Instagram jambo ambalo lilizua maswali kwa mashabiki juu ya ukimya wake.
Kwa hiyo siku ya jana alifanikiwa kuachia Minitape yake ambayo inangoma nane huku akiwaalika mastaa kama Jux, Ebitoke, Nedy Music, Mwijaku, Shetta na Barnaba kuhudhuria tukio hilo.
Mzee Yusuph alitangaza kuacha muziki miaka mitano iliyopita ila siku jana ameweza kurudi mjini kwa mara na kutoa nyimbo mpya na kufanya show mbele ya mamia ya watu walijitokeza huku akisema Taarab haijafa bali watu walimiss uwepo wake.