
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa daraja la JPM
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Mei 7, 2022 Jijini Mwanza mara baada ya kubaini upungufu wa wafanyakazi 200 katika ujenzi wa daraja hilo lenye urefu wa kilometa 3.2 ambalo limegharimu zaidi ya shilingi bilioni 600.
Ujenzi wa daraja la JPM unatekelezwa na kampuni ya kichina ya CCECC ambayo pia inatekeleza ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR ambapo Waziri Mkuu Majaliwa ameitaka kampuni hiyo kuacha tabia ya kuwapa ajira wafanyakazi wa daraja kwenye ujenzi wa reli na badala yake wabaki kumalizia ujenzi wa daraja hilo.
Katika hatua nyingine Mbunge wa jimbo la Sengerema Hamis Tabasamu, amemueleza Waziri Mkuu kuwa malipo ya wafanyakazi hao ni madogo hali inayopelekea wengine kuamua kuondoka.