Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, ACP Richard Abwao
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao, amesema kuwa tukio hilo limetokea Oktoba 24, 2021, na taarifa za kujinyonga kwa kijana huyo zilitolewa na dada wa marehemu aitwaye Jane Paul.
Kamanda Abwao amesema marehemu kabla ya kujinyonga aliacha ujumbe wa maandishi uliosomeka "Mama naomba unisamehe ni maisha tu yamenifanya nijiue mnizike''.
Chanzo cha tukio kimetajwa kuwa ni msongo wa mawazo, na mbinu aliyotumia ni kujifungia chumbani kisha kujitundika juu ya kenchi kwa kutumia shuka.