Jumanne , 5th Jul , 2022

Mtoto wa kike (5) mkazi wa Soga wilayani Kibaha mkoani Pwani ambaye jina lake limehifadhiwa, amejeruhiwa vibaya na mfanyakaz wa ndani aliyejuljkana kama Rehema baada ya kumwagiwa mafuta ya moto sehemu mbalimbal za mwili wake na kisha mtuhumiwa huyo kutoroka kusikojulikana.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Gregory Mushi

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Gregory Mushi, na kusema mtuhumiwa huyo alitenda jinai hyo majira ya saa 11:00 alfajiri na baada ya kutenda tukio hilo alifanikiwa kukimbia akipewa msaada wa baba mzazi wa mtoto huyo na kukimbilia kusikojulikana. 

Hata hivyo jeshi la polisi limefanikiwa kumkamata baba mzazi wa mtoto huyo kwa kosa la kumtorosha mtu aliyemjeruhi mtoto wake.