Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Kauli hiyo ameitoa leo Mei 16, 2022, bungeni jijini Dodoma, wakati wa uwasilishaji wa makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2022 hadi 2023 na kusema hadi sasa asilimia 95.8 ya wanannchi waliokuwa wanatumia dawa za ARV walikuwa wamefubaza wingi wa virusi vya Ukimwi ambayo ni sawa na chini ya nakala 1000.
"Hadi Desemba 2022, nchi yetu inakadiriwa kwamba kuwa na watanzania milioni 1.7 ambao wanaishi na virusi vya Ukimwi," amesema Waziri Ummy
Aidha Waziri Ummy, amemshukuru Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kwa kuwa balozi wa kuhamasisha wanaume kupima virusi vya Ukimwi.