Jumamosi , 23rd Oct , 2021

Jeshi la Polisi mkoa wa Njombe linawashikilia raia 52 kutoka nchi za Ethiopia na Malawi wanaodaiwa kuingia nchini bila ya kufuata utaratibu wakijaribu kuvuka mipaka kuelekea nchini Afrika Kusini.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe, Khamis Issah

Akizungumza mara baada ya kuwakamata raia hao, Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe, Khamis Issah, amesema kuwa watu hao wameharibu tu bajeti ya Taifa, kwani wamekula chakula ambacho hakikuwa kwenye bajeti yao.