Jumatatu , 28th Dec , 2015

Waziri wa nchi Sera, Uratibu, Bunge, ajira na Walemavu Mh. Jenista Mhagama amewatembela na kuwafariji waathirika wa majanga ya mvua zinazoendelea kunyesha ambazo zimeharibu nyumba za wananchi na kuwaacha bila makazi ya kuishi mkoani Ruvuma.

Waziri wa nchi sera,uratibu na Bunge ,ajira na Walemavu Mh. Jenista Mhagama amewatembela na kuwafariji wwaathirika wa Majanga ya mvua

Maeneo yaliyotembelewa na waziri huyo ambaye pia ni mbunge wa Peramiho Mkoani Ruvuma ni pamoja na kata ya Magagura ambapo ametoa msaada wa shilingi laki 9 kwa kata hiyo pamoja na kata ya Mbinga Mharule.

Akiongea na wakazi wa vijiji hivyo baada ya kukumbwa na maafa hayo Bi. Jenista ameagiza kupandwa kwa miti ili kujikinga na upepo na kupunguza athari za majanga kama hayo ya mvua.

Katika matukio hayo watu kadhaa walijeruhiwa ikiwemo mama na mwanae ambao waliangukiwa na ukuta wa nyumba yao ambapo baadhi ya wananchi walioathirika na maafa hayo wamehifadhiwa katika nyumba za serikali.