Alhamisi , 16th Nov , 2017

Aliyekuwa Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo ambaye sasa hivi ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo ajiunga na CCM.

Taarifa ya Kitila Mkumbo kujiunga na CCM imetolewa na uongozi wa chama mkoa wa Singida, huku ukituma ujumbe maalum wa kumkaribisha.

Hivi karibuni Kitila Mkumbo alitangaza kujivua uanachama wa ACT Wazalendo akisema kwamba kitendo cha kuwa mwanachama wa ACT Wazalendo na kuwa Katibu Mkuu wa Wizara kuna mgongano wa kimaslahi, hivyo ni vyema ajiondoe kwenye ACT Wazalendo.

Usome hapa chini