Jumanne , 26th Jan , 2016

Serikali imesema ili kukabiliana na tatizo la ajira kwa wahitimu wa elimu ya juu ambao wengi wao ni vijana imeandaa mpango maalumu ikiwa ni pamoja na kuimarisha wakala wa huduma za ajira nchini Tanzania (TAESA).

Naibu waziri wa Nchi Bunge Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Anthony Mavunde

Hayo yamesemwa leo Bunge na Naibu waziri wa Nchi Bunge Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Anthony Mavunde ambapo amesema wakala huwa utaweza kutimiza jukumu lake ipasavyo la kuwaunganisha watafuta kazi na waajiri wa ndani na nje ya nchi.

Aidha Mhe Mavunde ameongeza kuwa mpango mwingine ni pamoja na kuandaa mkakati wa kukuza ujuzi nchini ambao utaanza kutekelezwa mwaka ujao wa fedha 2016/2017 ambao utajikita zaidi katika kuwezesha mafunzo ya vitendo mahali pa kazi.

Mhe. Mavunde alikuwa anajibu swali la mbunge wa Vwawa Mhe Japhet Ngailonga Asunga ambaye alitaka kujua mpango wa serikali katika kujua idadi ya wahitimu wa elimu waliokosa ajira na mpango wa kuwawezesha kupunguza tatizo la ajira kwa wanaomaliza elimu ya juu.