Moja ya choo kinachotumiwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Kisaula
Shule ya Msingi Kisaula ina wanafunzi zaidi ya 130 ikiwa haina wanafunzi wa darasa la pili na darasa la nne kutokana na uhaba wa watoto wa kujiunga na madarasa hayo pindi walipokuwa wanaandikisha kuanza mikondo hiyo ya madarasa.
Kutokana na kuwepo kwa changamoto lukuki zinazoikabili shule hiyo wanafunzi wanalazimika kutumia vyoo vya asili kwa ajili ya haja ndogo na vingine kwa ajili ya haja kubwa, kutokana na kutokuwepo kwa vyoo bora shuleni hapo ambapo pia walimu nao wanalazimika kukaa nyumba moja jinsia tofauti.