Taarifa za awali kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Rweje katani hapo wamesema walishindwa kukadiria idadi ya tembo hao kwakuwa waliweka Nanga kijijini hapo kwenye nyakati za usiku wa saa tano wakitafuta chakula na kupiga kelele nyingi, ambapo asubuhi wamegundua uharibifu uliofanywa na wanyama hao ni pamoja na kula mahindi ambayo hayajavunwa, mtama na korosho.
Tembo hao wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 50 wameonekana katikati ya kijiji cha Rweje na Mkoka mida ya saa moja asubuhi wakiwa wanaelekea porini