Mkuu wa Mkoa wa Kegera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa watumishi hao hewa wamebainika kutokana na na taarifa ya timu ya uchunguzi ya kubaini watumishi iliyoundwa mkoani humo.
Pia, Meja Jenerali Kijuu, amesema kuna kiasi kidogo cha fedha ambacho wamefanikiwa kukirejesha serikalini lakini hali hiyo ya kusuasa kwa marejesho hayo inatokana na watumishi hewa kutopatikana ingawa bado wanaendelea kuwasaka.
Aidha, Jenerali Kijuu amesema kuwa baada ya kukamilika kwa ukaguzi huo ambao ameuita wa awali itaundwa tume nyingine itakayozunguka kwenye halmashauri na katika kila Kata ili kujiridhisha juu ya taarifa hizo.