Jumatatu , 27th Feb , 2017

Rapa Dogo Janja ambaye anafanya vyema na wimbo wake 'Kidebe' amefunguka na kumuomba Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Paul Makonda kuanzisha kampeni nyingine ya wezi wa vipuli vya gari.

Dogo Janja anasema kutokana na namna Mkuu wa Mkoa alivyoweza kusimamia vyema suala la madawa ya kulevya anaamini kuwa kiongozi huyo anaweza kuanzisha kampeni nyingine ya wezi wa vipuli vya magari ambao wanazidi kuongezeka mjini na kuwaliza.

Dogo Janja amesema hayo baada ya wezi hao kumliza kwa kuiba vitu kwenye gari yake. 

"Mheshimiwa Makonda tunashukuru umelisimamia vizuri suala la madawa ya kulevya na tumeona matunda yake. Lakini bado kuna hili la hawa wezi wa vipuli vya magari kama taa, radio, power window, naona kama alijaongelewa hivi. Hawa jamaa wapo wengi sana mjini na wanajulikana wanakuibia halafu wanakupigia simu wapi pakuvipata vitu vyako. Mheshimiwa tuanzishe na kampeni hii tupunguze kutiana hasara..ki-gari changu chenyewe ndiyo hiki natafutia riziki jana usiku wamekuja wameiba kila kitu radio, taa za mbele na nyuma, nitatokaje kujitafutia riziki? Alihoji Dogo Janja

Hiki ndicho alichopost Dogo Janja