Alhamisi , 28th Jul , 2016

Msanii wa kizazi kimpya Pamela alimaarufu kama Pam D amevunja ukimya na kusema anaumizwa na kuona wanaume wanawaogopa mastaa wa kike kwa kudhani ni wasaliti.

Pam D

Pam D alisema “Ukiachilia mbali mziki wangu ambao bado sijafikia levo amabazo nataka lakini kama msichana nilitamani kuwa katika strong relationship kitu ambacho nimekikosa kwani wanaume wengi wanaogopa wasichana maarufu wakihisi sisi ni wasaliti”

Hata hivyo Pam D hakusita kusema kuwa “Kama ikitokea nikapata mwanaume kama Nay wa Mitego itakuwa vizuri sana kwa sababu ni mtu ambaye anajielewa na
anakujenga, unapanuka kimawazo na anakufanya unakuwa strong kama alivyo yeye true boy ”. Pia Pam D alisema ni yupo tayari kufunga ndoa na Nay.