Jumanne , 26th Aug , 2014

Kikundi maarufu cha wasanii wa muziki nchini 'Mkubwa na Wanawe' aka Yamoto Band kipo mbioni kuzindua kichupa chao kipya kilichobatizwa jina 'Niseme Nisiseme'.

meneja wa TMK Wanaume Family Said Fella akiwa na Mkubwa na wanawe 'Yamoto band'

Meneja wa kundi la TMK Wanaume Family na kituo cha Mkubwa na Wanawe, Said Fella ameongea na eNewz kuwa hii ni moja ya video mpya inayotarajiwa kutambulishwa wiki hii ndani ya Tinga' Namba Moja kwa Vijana (EATV) iliyofanywa na watayarishaji mahiri Pablo na Iri.

Fella ameongezea kuwa uzinduzi wa wimbo huo utafanyika Jumapili Jijini Dar es Salaam ambapo pia wamepanga kutoa "Surprize" nyingi kwa mashabiki wao na pia listi nzima ya wasanii watakao perform siku hiyo itatangazwa wiki hii.