Jumatatu , 2nd Mei , 2016

Producer Frag kutoka Uptown Music ametumbua jipu baada ya kuibuka na kusema kuwa yeye ndiye aliyetengeneza wimbo wa Bado wa Harmonize na Diamond.

Producer kutoka Uptown Musi Fraga

Frag aliiambia Enewz kuwa pamoja na kazi kubwa aliyoifanya kuhakikisha ngoma hiyo inakuwa poa lakini bado WCB wakamzima na hawakumlipa hata senti tano na kuambulia elfu thelathini pekee ya nauli.

“Kawaida nikifanya kazi uptown music lazima saini zangu ziwepo lakini kwa kule wasafi saini zangu hazikuwekwa, na sijajua kwasababu gani hazikuwekwa wangeweka tu ata ile saini ya jina langu ili kunitengezea heshima kwa watu wengine ”, alisema Frag.