Jumatatu , 11th Jul , 2022

Ifikapo Novemba 15 mwaka huu idadi ya watu duniani itafikia bilioni 8 kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa, Idara ya Uchumi na Jamii siku ya leo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo idadi ya watu duniani inaongezeka kwa kasi ndogo zaidi tangu mwaka 1950.

Mwaka 2023 nchi ya India itaipita China kwa kuwa na idadi ya watu wengi duniani. 

Dunia itakuwa na watu bilioni 8.5 ifikapo 2030, na itafikia watu bilioni 9.7 ifikapo 2050. Na kabla ya 2080 idadi ya watu duniani itakua imefikia bilioni 10.4