Jumatatu , 5th Feb , 2024

Kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika kwenye miaka ya hivi karibuni nchini Marekani, zimebaini kuwa takribani nusu ya vijana wote nchini Marekani walio kati ya umri wa miaka 18 hadi 29 bado wanaishi na wazazi wao.

Sababu kuu ambayo imetajwa kwenye tafiti hiyo ni uchumi, huku pesa kidogo ambayo vijana wanapata wameonekana kuitumia kwenye maswala ya usafiri na bidhaa za anasaa (Vilevi, simu za bei mbaya, vishkwambi, Laptop kali nk.)

Lakini pia utafiti huo ulibaini kuwa gharama za kupangisha chumba/nyumba zimekuwa zikipanda kwa kila mwaka hali inayowafanya vijana hao waendelee kubana matumizi kwa kuishi kwa wazazi wao.