Alhamisi , 4th Apr , 2024

Muimbaji wa Nigeria Bella Shmurda amezua gumzo mitandaoni baada ya kusema hata akiulizwa nani amemsaidia kwenye maisha yake atamtaja Boss wa YBNL Nation, rapa Olamide kwanza halafu mama yake ndio atafuata.

Picha ya Bella Shmurda kushoto na Olamide upande wa kulia.

“Hata watoto wangu wakiniuliza ni nani aliyenisaidia, nitamtaja Olamide kwanza kabla sijamtaja mama yangu.Olamide ni namba 1 kuliko mtu yeyote”.

Bella Shmurda ambaye anafahamika kwa jina lingine la mtoto wa kwanza wa Olamide tayari ameshafanya nyimbo mbili na Olamide ambazo ni Vision 2020 na Triumphant.

Unaweza kumtupa mzazi wako mbele ya mtu baki kwa msaada aliyekupa?