Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Msako mkali kwa waajiri wasiotoa mikataba

Alhamisi , 6th Oct , 2022

Kampuni, taasisi na viwanda ambavyo havitoi mkataba kwa waajiriwa wataanza kuchukuliwa hatua baada ya Serikali kuanza kutangaza msako kwa waajiri.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya wiki ya vijana inayotarajia kuanza Oktoba 8, 2022.

Katambi amesema kwa muda mrefu wamekuwa wakihamasisha waajiri kutoa mikataba kwa wafanyakazi wao jambo ambalo utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua katika baadhi ya maeneo.

"Kuna baadhi ya maeneo waajiriwa hawana mikataba, wengine wana mikataba ambayo haijaandikwa ukomo wake, linapotokea jambo wanaenda kujaza tarehe ya mwisho ya ukomo ili kumtoa muhusika katkka ajira jambo ambalo halikubaliki,"

Amebainisha kuwa kukosekana kwa mikataba imekuwa ikiweka ugumu kwa waajiriwa kudai haki zao pindi wanapoppteza ajira.Pia, amesema baadhi ya waajiri wanatoa mishahara iliyo chini ya kima cha chinj cha mshahara kilichowekwa na Serikali jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Katika hatua nyingine, Katambi amesema Katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2022, Serikali imeendelea kufanya kaguzi za utekelezaji wa sheria nchini ambapo jumla ya kaguzi 859 zimefanyika katika maeneo ya kazi na waajiri waliokiuka Sheria kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria.

Pia wizara imeendelea kuratibu ajira za wageni kwa kutoa vibali vya kazi ambapo 3,298 vimetolewa, makusanyo ya maduhuli yanayotokana na vibali vya kazi na leseni za wakala wa ajira vimefikia Sh8.69 bilioni.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu