Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Precision Air msafirishaji 'KARIBU-KILIFAIR 2022'

Jumatano , 4th Mei , 2022

Shirika la ndege linaloongoza Tanzania, Precision Air ndio msafirishaji rasmi wa maonyesho ya utalii ya kimataifa yanayoitwa ‘KARIBU-KILIFAIR 2022’, ambayo yatafanyika Arusha kuanzia Juni 3 hadi 5.

Maonyesho haya ambayo yatafanyika kwa mara ya kwanza baada ya kusitishwa kwa miaka miwili kutokana na janga la Uviko-19, yanategemea kuvutia washiriki kutoka Afrika mashariki na wanunuaji kutoka masoko ya kimataifa.

Akizungumzia ufadhili huo, Meneja masoko na mawasiliano wa Precision Air, Bw. Hilary Mremi alisema, Precision Air inajivunia kuwa sehemu ya maonyesho hayo ambayo yatakuza utalii nchini Tanzania.

“Tunafurahi kwa mara nyingine tena kuwa sehemu ya maonyesho haya muhimu kwa ajili ya utalii wetu, sisi kama wadau wakubwa wa utalii nchini tunawajibika  kuunga mkono matukio ya aina hii. Tunaamini kupitia ufadhili huu kwa KARIBU-KILIFAIR tutakuwa tunamuunga mkono Rais wetu, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika juhudi zake za kuitangaza nchi yetu duniani” aliongeza.

KARIBU-KILIFAIR ni muunganiko wa maonyesho mawili ambayo ni KARIBU FAIR na KILIFAIR, maonyesho haya yamevuta zaidi ya washiriki 450 kutoka Afrika mashariki, wanunuzi 600 kutoka duniani kote na zaidi ya wahudhuriaji 7000 ndani ya siku tatu. Mwaka huu maonyesho haya yatafanyika katika viwanja vya Magereza mkabala na kiwanja cha ndege cha Arusha kuanzia Juni 3 hadi 5, 2022.

Akizungumzia udhamini huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kilimanjaro Promotion Bw. Dominic Shoo alisema,”Tukio hili linalenga kujenga biashara na kufanya wadau wa utalii kukutana baada ya changamoto ya muda mrefu ya Uviko-19. Tukio la mwaka huu limevuta hisia kubwa kutoka kwa wadau jambo ambalo linaonyesha kuwa watu wana hamu ya kukuza biashara zao zaidi ya hapo awali.

Akifafanua zaidi, “Tunawashukuru sana Precision Air kwa msaada wao. Kupitia ushirikiano wao, tukio letu limekuwa na mafanikio kila mwaka”.

Precision Air ni kampuni ya ndege ya Kitanzania inayofanya safari zake kutoka makao yake makuu Dar es salaam kwenda Arusha, Bukoba, Dodoma, Kahama, Kilimanjaro, Mbeya, Mtwara, Tabora, Mwanza, Seronera(Serengeti), Zanzibar na Nairobi.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava