Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania yapewa uhuru na Kenya

Jumatano , 5th Mei , 2021

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, ametoa uhuru wa kibiashara kwa wawekezaji wa Tanzania kuwekeza nchini Kenya bila kuwa na visa za biashara wala kibali cha kazi na kuwasihi wahakikishe wanazingatia sheria na kanuni zinazofuatwa na wawekezaji wa Kenya.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta

Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 5, 2021, nchini Kenya wakati wa ufunguzi wa kongamano la wafanyabiashara wa Kenya na Tanzania ambalo wamelifungua kwa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, na kuongeza kuwa watahakikisha wanarahisisha njia zote za ufanyaji biashara.

"Tungependa kuona wawekezaji wengi wa Tanzania waje wafanye kazi zao hapa Kenya, wawekezaji wa Tanzania mjue kwamba mko na uhuru wa kuleta na kufanya biashara zenu hapa bila kuombwa 'business visa' na work permits' ila mfuate sheria na kanuni zilizowekwa na zile ambazo wenzenu wa Kenya pia lazima wazifuate", amesema Rais Kenyatta

Awali pia Rais Kenyatta akasisitiza umuhimu wa kushirikiana na siyo kushindana, "Tuko na nafasi na nia ya kuhakikisha kwamba tukifanya pamoja tunaweza kuinua uchumi wa Tanzania na Kenya, naamini Mh Rais Samia Suluhu, kwa dhati ya kwamba tukiingia kwa njia ya kushirikiana ushindi utakuwa wa wananchi wa nchi zetu".
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa