Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vodacom kuwaongezea miamala wateja

Jumatano , 10th Jul , 2019

Kampuni ya Mawasiliano ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, imeanzisha huduma inayomuwezesha mteja, kuongezewa muamala wa pesa pindi anapopungukiwa.

Mkurugenzi wa M-pesa Epimark Mbeteni.

Akizungumza Jijini Dar Es Salaam, Mkurugenzi wa M-pesa Epimark Mbeteni amesema, huduma hiyo imekuja kwa kushirikiana na benki ya TPB, na kwamba ushirikiano huo utaweza kutatua matatizo ya kifedha yanayojitokeza.

''Hii ni huduma ambayo itaweza kumsaidia mteja kukamilisha muamala uliopungua, wakati wa kununua Luku, kutuma pesa, au wakati wa kununua bidhaa mbalimbali''.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Benki hiyo, Mkurugenzi wa vihatarishi wa TPB, Mosses Manyata amesema, huduma hiyo iliyopewa jina la Songesha na M-pesa, ni mtatuzi wa matatizo ya ghafla kwa mteja, wakati wa kutuma pesa ama kulipia bili mbalimbali.

Hii ni mara ya pili sasa kwa Kampuni ya Vodacom, kuungana na Benki hiyo, na kutoa huduma inayohusisha na kugusa maisha ya watanzania wengi.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji