Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 10, 2022, mara baada ya kuwaapisha Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu na Makatibu Wakuu wasaidizi Ikulu ya Chamwino Dodoma, na amewachukua hao wawili kwa lengo la kuwasimamia viongozi wengine kwani tayari wao wameshafikia umri wa kustaafu.
"Kaka yangu Lukuvi ana kazi na mimi, nimeona meseji nyingi nyingi, afadhali Lukuvi ametoka, hajatoka yupo, wengine wameanza kumletea meseji za ajabu wakijua atagombania Uspika, hatagombania ana kazi na mimi, msianze kumchafua, ametumikia Taifa hili kwa uadilifu, mwache aende na mimi tumalize kazi," amesema Rais Samia