Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ahadi ya RC Makonda kwa kijana Hamis

Ijumaa , 15th Mar , 2019

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo amemtembelea na kumjulia hali kijana Hamis Hashim aliyelazwa katika Hospital ya Taifa Muhimbili akisumbuliwa na tatizo la miguu kuvimba hadi kuzidi uzito wa mwili, ambapo ameahidi kusaidia gharama za matibabu iwe ndani au nje ya nchi.

Paul Makonda akimjulia hali kijana Hamis, hospitali ya taifa Muhimbili.

Aidha RC Makonda amesema kwa sasa hali ya Afya ya Hamis inaendelea vizuri baada ya madaktari bingwa wa Muhimbili kuendelea kuchukuwa vipimo kwa umakini wa hali ya juu. Pamoja na hayo RC Makonda amemkabidhi Kijana Hamis kiasi cha shilingi laki tano kwaajili ya kununua chakula kwa siku atakazokuwa Hospital.

Kwa upande wake Hamis Hashim amemshukuru RC Makonda kwa moyo wa huruma aliokuwa nao ambapo ameeleza kuwa amekuwa anaishi maisha ya tabu lakini kwa sasa anajisikia faraja kuona RC Makonda ameahidi kumsaidia kwa kila jambo.

Kwa Mujibu wa Dr. Ibrahim Nkoma ambaye ni Mkuu wa idara ya upasuaji hospital ya taifa Muhimbili anasema Hamis Hashim anasumbuliwa na tatizo la neva za fahamu kukuwa kupita uwezo.

RC Makonda baada kuona taarifa za kijana Hamis kapitia mitandao ya kijamii aliguswa na juzi aliagiza apelekwe hospital kwaajili ya kuchukuliwa vipimo ambapo licha ya Hamis kuugua pia anaishi katika Familia ya hali ya chini akimtegemea Mama mzazi ambaye naye hana kazi baada ya Baba mzazi kufariki.

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90