Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Alichokisema JPM kwa waliozusha kifo cha Mpango

Ijumaa , 19th Feb , 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, amewataka Watanzania kuacha kutiana hofu na badala yake wawe na umoja yanapotokea matatizo, hii ni baada ya mitandao ya kijamii kuzusha kwamba Waziri wa Fedha Dkt. Philip Mpango, amefariki dunia taarifa ambazo amezikanusha.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli

Kauli hiyo ameitoa hii leo Februari 19, 2021, wakati akiongozi familia, viongozi wa dini na wananchi waliojitokeza kuaga mwili wa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, aliyefariki dunia Februari 17, 2021, na ndipo alipoamua kuusoma hadharani ujumbe alioandikiwa na Waziri huyo.

"Tumefikia mahali sasa tunatishana sana, leo nilitumiwa meseji na Waziri wa Fedha Dkt. Mpango, ambaye amelazwa Dodoma, na ninaomba niusome hapa kwa faida ya wale ambao walikuwa wana-Tweet kwamba amekufa na amenitumia leo asubuhi", amesema Rais Dkt. Magufuli

Aidha Dkt. Magufuli, aliendelea kuusoma ujumbe huo, "Ameniambia Mh. Rais asante sana nimepata ujumbe wako kupitia kwa mke wangu, kwa Neema ya Mungu naendelea vizuri, nakula na ninafanya mazoezi ya kifua na kutembea hao wanaonizushia kifo niliwaombea msamaha kwa Yesu wakati wa sala ya jioni jana, Mungu akubariki na akupe Neema na ujasiri zaidi katika kuliongoza Taifa letu katika wimbi hili".

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava