Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ashtakiwa kwa kumbaka mtoto wake wa miaka 4

Jumapili , 16th Dec , 2018

Mwanaume mmoja aliyejulikana kwa majina ya Mmanga Mrope (47), amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tunduru kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka minane, mtoto ambaye alikuwa akimlea. 

mtu akiwa rumande

Wakati akisomewa mashtaka hayo, Desemba 14 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Abdalah Amwero, mwendesha mashtaka Inspekta Steven Msongaleli alidai kuwa kwa mara ya mwisho mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Desemba 6, mwaka huu, majira ya saa 4.40 usiku baada ya kumvamia na kumziba mdomo mtoto huyo na kufanikisha azima yake.

Msongaleli alidai kuwa mtuhumiwa huyo alianza tabia ya kumwingilia mtoto huyo anayesoma darasa la tatu (jina la shule linahifadhiwa) pamoja na kumfanyia kitendo hicho kinyume cha maumbile katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

Alisema kwa kufanya hivyo Mrope alifanya kosa kinyume cha sheria namba 130 (1) na (2c) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura namba 16 kama ilivyofanyiwa mabadiliko mwaka 2002.

Mtuhumiwa huyo alibainika baada ya mtoto kumwambia mwalimu wake wa darasa baada ya kumhoji kutokana na mtoto huyo kuonekana kukosa furaha wakati wote anapokuwa shuleni, ambapo baada ya kubaini hivyo, walimu walimuhoji mtoto huyo na kuwaeleza kuwa mtuhumiwa alikuwa akimtishia kumuua na kukimbilia nchi jirani ya Msumbiji endapo angetoa siri.

Mtoto huyo alipelekwa katika hospitali ya wilaya ya Tunduru kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na vipomo kuthibitisha iwapo alifanyiwa kitendo hicho. Mwendesha mashtaka amedai kuwa baada ya vipimo kubaini hivyo, ndipo mtuhumiwa alikamatwa.

Mtuhumiwa amekana kufanya kosa hilo na kupelekwa rumande baada ya kukosa wadhamini. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 18 kwa ajili ya kusikilizwa tena.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto