Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ataka mgao wa mali za Hayati Kibaki

Ijumaa , 20th Mei , 2022

Mwanamume mmoja nchini Kenya Jacob Ochola ameibuka na kudai mgao wa mali za aliyekuwa Rais wa tatu wa Kenya Mwai Kibaki akieleza kuwa yeye ni mtoto wa kwanza wa Kibaki.

Jacob Ochola

Ochola anadai kuwa akiwa na miaka 21 alifahamishwa kuwa Kibaki ni baba yake na wakaanza kuwa na mahusiano mazuri

Anasema mama yake aliolewa akiwa mtoto mdogo na ndio maana jina lake la ukoo linatoka katika jamii ya Wajaluo. 

Katika mahojiano na chombo kimoja cha habari nchini Kenya Ochola anasema baada ya kifo cha baba yake mlezi, ndipo mama yake alimfahamisha kuwa marehemu si baba yake mzazi.

"Nilizaliwa Julai 22, 1960, Kaloleni, Nairobi. Nilikua nikijua mimi ni Mluo. Nilikuja kujua kwamba sikuwa Mjaluo nilipofikisha miaka 21. Mwaka mmoja baada ya mtu niliyemfahamu kuwa ni baba yangu kufariki, mama yangu alinieleza kuwa aliyefariki si baba yangu mzazi, aliniambia pia anaenda kuongea na baba yangu kwa sababu anataka kuniona alifanya hivyo baada ya mwezi mmoja hivi. Huu ndio wakati nilipata fursa ya kukutana na rais wa zamani," amenukuliwa Ochola 

Aidha ameeleza kuwa wakati Mwai Kibaki akiwa hai alikuwa akimtembelea mara kadhaa kwa siri katika hoteli moja nchini Kenya na kuonana naye

Hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na upande wa familia ya Rais huyo wa zamani wa Kenya kuhusu mtu huyo 

Vyanzo vya habari nchini Kenya vinadai mali za kiongozi huyo zina  thamani ya KSh150 bilioni ambapo mwanaume huyo anasema anahitaji kujumuishwa katika mgao wa mali hizo

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava