Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ataka Tume ya Uchaguzi iwe kama CAG

Jumanne , 14th Mei , 2019

Mwanaharakati Bob Chacha Wangwe amependekeza Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC), kupewa nguvu ya kikatiba kama aliyopewa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali CAG, ili aweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Chacha Wangwe ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast cha East Africa Radio, ambapo amesema endapo akipewa nguvu hiyo itamlinda kikatiba.

"Tumependekeza kuwepo kwa mfuko maalum ambao utawafanya Tume ya Uchaguzi kujiendesha na sio mpaka kuomba Serikali kuu, pia tunapendekeza kiongozi wa Tume apewe ulinzi wa kikatiba kama ilivyokuwa kwa CAG ambaye anaweza kupambana na watu wakubwa kama Spika Ndugai." amesema Bob Chacha Wangwe.

"Kwa muundo uliopo sasa hivi, Wakurugenzi wengi walikuwa ni wagombea Ubunge ambao walishindwa, na wengine ni makada wa vyama vya siasa", ameongeza Bob Chacha Wangwe.

Hivi karibuni Bob Chacha Wangwe alifungua kesi Mahakama kuu ya Tanzania kupinga sheria inayowapa mamlaka Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia uchaguzi huku wakiwa na mahusiano na vyama vya siasa, kesi ambayo Mahakama ilimpa ushindi lakini kupitia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jamhuri imekata rufaa.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava