Martin Kinasa aliyeuawa
Baadhi ya ndugu wa marehemu akiwemo Peter Kinasa wakizungumza na EATV amesema kuwa, "Ndugu yetu aliuawa na bodaboda baada ya kupata idhini kutoka kwa polisi kuwa tukamatieni huyo mtu anayekuja huko ni mwizi wa pikipiki, kwahiyo hiyo hali ndio ilisababisha ndugu yetu akatoka duniani"
Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza Wilbroad Mutafungwa, akizungumza kwa sharti la kutopigwa picha, amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo lililotokea Desemba Mosi mwaka huu katika kijiji cha Nyagili, Kata ya Chabula wilayani Magu.